Thursday , 20th Oct , 2022

Thamani ya soko la hisa la Dar es salaam imeshuka Kwa asilimia 0.71na kufikia shilingi trilioni 15.28 ikilingaishwa na thamani ya soko Hilo katika juma lililoishia Octoba saba ambapo ilikuwa na thamani ya shilingi trilioni 15.39

Akitoa taarifa ya mwenendo wa soko la la hisa la Dar es salaam Afisa maendeleo ya Biashara DSE Leonard Kameta amesema kushuka Kwa thamani ya soko Hilo kumesababishwa na kushuka Kwa bei za hisa katika kampuni za NMG,KCB,EABL na JHL

Katika robo ya nne ya mwaka  mpaka Sasa wawezekaji wa ndani wamechangia asilimia 98.14 ya uwekezaji wote huku wawezekaji wa nje wakichangia asilimia 1.86 ya uwekezaji

Katika wiki iliyoishia Octoba 13 miamala iliyofanyika kwenye upande wa hatifungani ina thamani ya shilingi bilioni 28.30  ikikinganishwa na miamala yenye thamani ya shilingi bilioni 120 Kwa juma lililoishia Octoba Saba