Wednesday , 19th Oct , 2022

Vyama vya ushirika nchini vimetakiwa kutumia fursa ya kuwekeza kwenye uzalishaji wa  mazao  ya Miwa na Alizeti ambayo serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kuagiza Sukari na Mafuta nje ya nchi kutokana na uzalishaji wa ndani kutokutosheleza hatua itakayo saidia kukuza uchumi.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Kilimo Antony Mavunde, akiwa mkoani Mwanza katika Kongamano la wanawake wa ushirika wa akiba na mikopo Tanzania na kueleza ipo haja ya vyama vya ushirika kuwekeza katika uzalishaji wa mazao hayo muhimu ambayo uhitaji wake ni mkubwa.

Wanachama  wa ushirika wameeleza watachukua hatua kuwekeza katika maeneo yenye fursa zaidi za kukuza uchumi ikiwemo kilimo.