Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mizigo ya EABC kupewa kipaumbele bandarini

Friday , 23rd Sep , 2022

Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC) limeiomba mamlaka ya mapato Tanzania (TPA) kutoa kadi ya kijani kwa wanachama wake ili kuipa mizigo yake kipaumbele cha kutolewa bandarini haraka.

Bw. Plasduce M. Mbossa, Mkurugenzi Mkuu TPA

Mapema leo Septemba 23, 2022 wajumbe wa baraza la biashara la Afrika Mashariki (EABC) wamekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari ili kuona namna ya kuongeza kasi ya upakuaji na usafirishaji wa mizigo kutoka bandari ya Dar es Salaam kwenda katika mataifa yasiyo na bandari ikiwemo Malwai, Zambia, Congo, Burundi, Rwanda na Uganda.

“Sisi ndiyo washikadau mhimu katika bandari ya Dar es Salaam, hivyo baada ya kuteuliwa kwa Mkurugenzi mpya wa TPA tumeona ni vema tukutane na kuzungumza nae ili kujadili changamoto tulizonazo na ni kipi tufanye, mfano hapa bandarini kuna ucheleweshwaji wa upakuaji mizigo na kuutoa mzigo bandarini, tunatumia muda mrefu kukamilisha mchakato, hivyo tumemuomba kwamba sisi wanachama wa EABC ambao ndo wateja wakubwa kwa bandari tupewe kadi ya kijani ambayo itatoa kipaumbele kwa mizigo yetu ili ishughulikiwe haraka inapokuwa bandarini na kuchangamsha biashara"- John Bosco Kalisa, Mkurugenzi Mtendaji  EABC.  

Aidha, kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo Mkurugenzi wa TPA, Bw. Plasduce Mbossa amesema kuwa mamlaka hiyo na serikali wamepanga kuanza ujenzi wa bandari hiyo kwa pesa zake hata kama mfadhili atachelewa kupataikana na kwamba ikikamilika itaongeza ufanisi wa bandari za Tanzania.

“Hata hivyo ili kuhakikisha kwamba tunawahudumia wateja, suala la Bandari ya Bagamoyo ni mhimu, na mamlaka ya bandari na serikali  tutaanza ujenzi wa bandari ile bila kusubiri mfadhili, ikikamilika ile maana yake ni kwamba foleni katika bandari ya Dar es Salaam itapungua na wafanyabiashara hawatakimbia kwenda nchi zingine"- Plasduce Mbossa,  Mkurugenzi Mkuu TPA.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine