Tuesday , 12th Jul , 2022

Msanii Afande Sele amesema kazi zake ndio zimefanya kukutana na Mchungaji Antony Lusekelo (Mzee wa Upako) kwa sababu kazi zake zina maana kwenye jamii, ushawishi na vinaishi.

Picha ya Afande Sele na Mzee wa Upako

Akizungumza baada ya kukutana na Mzee wa Upako kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio, Afande Sele amesema

"Kazi zangu zimekuwa zina maana kwenye jamii, ushawishi na vinaishi. Mchungaji Lusekelo ni mtu wa imani na maono kikubwa ni kazi ndio zimetukutanisha, kila siku nawaambia wasanii watengeneze kazi zitakazowaletea wafuasi sio mashabiki".