Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Teknolojia mpya ya ‘Offside’ kutumika WC Qatar

Friday , 1st Jul , 2022

Shirikisho la Soka Duniani ‘FIFA’ limethibitisha kuwa litatuma teknolojia mpya yenye utaalam wa hali ya juu ya kutambua mchezaji atakayeotea ‘Offside’ kwenye michuano ya kombe la Dunia inayotaraji kuanza Novemba 21, 2022 Nchini Qatar.

Gianni Infantino - Rais wa FIFA

Teknolojia hiyo itahusisa uwepo wa ‘sensor’ yaani kifaa maalumu cha kuhisi kitu kitakachowekwa ndani ya mpira huku kikiwa na uwezo wa kutuma taarifa mara 500 kwa sekunde kwa kusoma uelekeo halisi wa mpira.

Mbali na ‘Sensor’, lakini kutakuwa na kamera maalumu 12 ambazo zitawekwa kwenye kila paa la uwanja kwa ajili ya kufuatilia mwendo wa kutoka kwenye mwili wa kila mchezaji kwa kutuma taarifa mara 50 kwa sekunde kwa mchezaji aliye na mpira kwa wakati husika.

Mchezaji yeyote akiwa kwenye nafasi ya kuotea ‘Offside’ taarifa ya tahadhari itatumwa katika chumba cha waamuzi wasaidizi kwa njia ya video ambapo waamuzi hao watatuma taarifa haraka kwa mwamuzi wa kati ili imsaidie afanye maamuzi.

Mfumo huo ulijaribiwa katika michezo ya kombe la Dunia la vilabu msimu wa mwaka jana ambapo ilikadiriwa kupunguza muda uliokuwa unatumiwa na VAR kufanya maamuzi ya ‘Offside’ kutoka sekunde 70 hadi sekunde 25.

Upande wa mkuu wa waamuzi wa FIFA, Pierluigi Collina alisema mfumo huo ni mzuri na sasa uko tayari kwa ajili ya kutumika na waamuzi. Michuano hiyo mikubwa ya soka Duniani itaraji kuanza 21 Novemba 2022 na kutamatika Desemba 18, 2022 nchini Qatar.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine