Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NAOT watoa msaada kwa watoto yatima Dodoma

Saturday , 25th Jun , 2022

Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wamekabidhi msaada kwa kituo cha watoto yatima kilichopo Kijiji cha Matumaini jijini Dodoma. Msaada huo umekabidhiwa kwa mlezi wa Kituo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo huadhimishwa mwezi Juni kila mwaka.

Akizungumza kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Naibu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali – Divisheni Serikali za Mitaa, Bw. Benjamin Mashauri amesema utoaji wa msaada huo ni sehemu ya hatua mbalimbali zilizopendekezwa katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2022.

“Kwa namna ya pekee naomba upokee salamu za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ambae anatambua kazi kubwa mnayoifanya katika kituo hiki ya kulea watoto na Ofisi yetu itaendelea kutoa misaada kwa jamii kadri itakavyowezekana,” amefafanua zaidi Mashauri. Msaada uliotolewa kwa kituo ni pamoja na mchele, sukari, maji ya kunywa, maziwa ya unga aina ya lacktojeni kwa watoto wachanga, sabuni za kufulia, sabuni za kuogea, mafuta ya kupikia, soda, juisi na zawadi nyingine za kuwapa watoto faraja.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ni moja ya matukio muhimu katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kufanya maonyesho ya kazi mbalimbali na Kongamano kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma. Moja kati ya shughuli zilizotekelezwa katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu ilikuwa ni pamoja na kufanya shughuli za kijamii ili kujenga mahusiano mazuri na Wananchi.


Kwa kutambua kwamba Kijiji cha Matumaini kinatoa mchango mkubwa katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha ustawi wa jamii hususani katika kulea na kutunza watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu. Mbali na kukabidhi msaada huo wa Ofisi, Wafanyakazi walioshiriki kwenye tukio hilo waliendesha harambee fupi na kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni 1 na laki 4 ambazo walizikabidhi kwa Kituo ili ziweze kusaidia mahitaji ya Kituo.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine