Thursday , 6th Jan , 2022

Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu, ameendelea kusisitiza kwamba wakuu wa shule kutoweka vikwazo kwa wanafunzi wataokuwa hawana sare za shule badala yake wawaruhusu kuingia darasani hata na sare zao waliuzokuwa wanavaa shule ya msingi.

Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januri 6, 2021, wakati akitoa tamkoa maalum kwa wanafunzi wanaotarajiwa kuanza masomo Januari 17, huku akimshukuru Rais Samia kwa kuwezesha ukamilikaji wa madarasa 12,000 nchini.

"Kama ni mwanafunzi wa sekondari anaweza akatumia sare yake aliyokuwa anavaa shule ya msingi wakati mzazi anatafuta fedha au akavaa tu t-shirt na sketi yake nzuri akaenda darasani, wazazi pia waangalie joining instruction (maelekezo ya kujiunga na shule) inasema nini kwa sababu kuna vitu vingi ambavyo havina hata umuhimu, jamani tuondoe vikwazo," amesema Waziri Ummy.