Baadhi ya wananchi Vijiji vya Halawa na Ihusi Bariadi mkoani Simiyu
Malalamiko hayo yametolewa kwenye mikutano ya hadhara katika vijiji hivyo, ambapo sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009 pamoja na itifaki za kikanda, zinazuia utumikishwaji wa watoto na kutoa kipaumbele cha elimu.
Kulingana na malalamiko ya wananchi, Diwani wa Kata ya Nkindwabiye, Safari Ng'habi, ametangaza uchunguzi juu ya suala hilo, huku Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Lupakisyo Andrea Kapange, naye akatoa onyo kwa walimu wanaowageuza wanafunzi kuwa vijakazi wao.