
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Ulrich Matei, akionesha bastola ya Mkuu wa Wilaya ya Sikonge
Taarifa hiyo imetolewa leo Agosti 4, 2021, na Kamanda wa Polisi mkoani humo Ulrich Matei, ambapo hata hivyo hakueleza mazingira yaliyosababisha bastola hiyo ya Mkuu wa wilaya kukutwa ikiwa mikononi mwa wahalifu.
Kamanda Matei amewataja watu waliokamatwa na bastola hiyo kuwa ni Isaka William (24), Farew Raphael (30), Malodi Joseph (24), Daniel Kamwela (24) na Shadrack Msemwa (35) wote wakazi wa Iyunga Jijini Mbeya.