Monday , 28th Jun , 2021

Nyota wa timu ya Milwaukee Bucks, Khris Middleton ameibuka kuwa nyota wa mchezo wa mzunguko wa tatu wa fainali ya ligi ya kikapu nchini Marekani ukanda wa Mashariki baada ya kupata alama 38, rebaundi 11 na assisti 7 na kuisaidia timuu yake kushinda kwa alama 113-102 dhidi ya Atlanta Hawks.

Nyota wa Clippers, Khris Middleton akitupia mpira kuisaidia timu yake kupata alama.

Middleton nouma, aibeba Bucks fainali NBAUshindi huo umewafanya Bucks kuongoza kwenye michezo yake miwili mbele ya Hawks wenye ushindi kwenye mchezo mmoja wakitegemea kuendelea kuchuana kuelekea michezo saba ya kuamua hatma ya ubingwa kwenye fainali hiyo.

Middleton amewashangaza wengi kwa kuwambwaga wakali kama vile chipukizi wa Atlanta Hawks, Trae Young na hata nyota mwenzake, Giannis Antetokounmpo.

Kwa upande wa Hawks, wapo njia panda kwani nyota wake Trae Young amepata maumivu ya kifundo cha mguu ambapo watalazimika kusubiri majibu ya MRI ili kubaini ukubwa au udogo wa maumivu hayo.

NBA itaendelea tena saa 10:00 Alfajiri ya kuamkia kesho kwa mchezo mmoja wa mzunguko wa tano wa fainali kwa ukanda wa Mashariki ambapo Los Angeles Clippers watachuana vikali na Phoenix Suns  mchezo ambao Suns akishinda atatwaa ubingwa wa ukanda huo.