Thursday , 24th Jun , 2021

Shirikisho la soka Ulaya (UEFA)imeondoa kanuni ya goli la ugenini katika mashindano yake kuanzia msimu ujao wa 2021/2022

Rais wa UEFA Alexander Ceferin

Kamati ya utendaji  ya UEFA , imeridhia  na kuthibitisha mapendekezo ya  kamati ya mashindano  kwa upande wa vilabu  vya wanaume na  vile vya wanawake kuondoa kanuni  ya faida ya goli la ugenini.

Rais  wa UEFA  Alexander Ceferin amesema “kanuni  hii  imekuwepo tangu mwaka 1965, kwa miaka  ya karibuni ilileta mjadala mkubwa sana,kufikia hapa ni sawa tumeshinda vita’’

‘’Tumefanya  utafiti na tukajiridhisha kwamba, kwa sasa kanuni hii imepitwa na wakati  imefikia mahala inaharibu hadi mbinu za ufundi wakati wa kucheza kwa kuwa timu inayocheza nyumbani inatumia muda mwingi kujihami badala ya kushambulia kwa kuhofia endapo timu ngeni itapata goli basi katika  mechi ya mkondo wa pili  itawanufaisha wapinzani’’ aliongeza Ceferine 

UEFA wamekuwa wakisimamia mashindano yao  ngazi  ya vilabu  kwa  upande wa  mabingwa Ulaya na ile ya ’ Europa League’pamoja na michuano ya vijana na wanawake,  kwa taarifa hii maana yake imefutwa kwa mashindano yote .