Tuesday , 25th May , 2021

Tarehe kama ya leo Mei 25,2018 msanii wa Bongo Fleva, Marioo aliachia wimbo wake wa 3 ‘Subira’ ikiwa ilikuwa ni siku ya 133 tangu aachie kazi yake ya kwanza  ‘Dar Kugumu’ Januari 13 iliyomtambulisha vizuri kwenye game.

Msanii Marioo

Wimbo huo uliendelea kumuweka katika nafasi nzuri kimuziki kutokana na mapokezi yake kuendelea kuwa makubwa, huku video  yake ilifanyika mjini  Morogoro na Dar es Salaam na kuongozwa na Frank Papushka na Hanscana brand, huku na audio ilitayarishwa na Kimambo.

Kwasasa Marioo ni miongoni mwa wasanii wa Bongo  wenye nguvu kubwa ya ushawishi ambapo amefanikiwa kufanya kazi na wasanii wakubwa wa nje ya Tanzania kama Sho Madjozi, Bontle Smith, Skales.