Rais Mteule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt Hussein Mwinyi.
Dkt Mwinyi anakuwa Rais wa nane wa taifa hilo tangu Mapinduzi Matukufu
	ya 1964, katika hotuba yake ya mwanzo mapema leo baada ya kuwa Rais
	mteule amewashukuru Wanzanzibar wote kwa busara zao na uvumilivu zaidi
	akiwataka kuja pamoja kulijenga taifa lao na kuziweka tofauti zao
	pembeni.
	''Niwashukuru zaidi kwa kunipigia kura za kutosheleza kutangazwa na tume
	kuwa Rais Mteule wa Zanzibar, ni imani kubwa kwangu na niwahakikishie
	nimeipokea imani hii kwa uzito mkubwa, kwa kuwa imani huzaa imani nami
	nitawalipa imani hii kwa utumishi uliotukuka'' - Dkt Hussein Mwinyi.
	Mwinyi ameongeza kuwa'' Aidha nitumie fursa hii kuwapongeza wagombea
	wenzangu wote tulioshiriki uchaguzi huu, nikiri kuwa nimejifunza mengi
	kutoka kwenu, nitatumia yale mazuri yenu mliyoshauri na mliyo ya ahidi
	maana lengo letu ni kuijenga Zanzibar, Zanzibar ni kubwa na muhimu
	kuliko tofauti zetu''.

