Friday , 9th Oct , 2020

Mgombea Ubunge jimbo la Ubungo kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Euegene Kabendera, amewataka wananchi wa Ubungo kumchagua ambapo ameahidi kuwa atahakikisha suala la ukosefu wa ajira linashughulikiwa kwa kufufua viwanda vilivyokufa.

Mgombea Ubunge jimbo la Ubungo kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Euegene Kabendera

Akizungumza  hii leo na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam, mgombea huyo amesema kuwa anafahamu kuwa jimbo hilo linakabiliwa na changamoto ya ajira na kudai kuwa vijana wengi wengi wa Ubungo hawana ajira na kuahidi kurudisha viwanda vilivyokufa ili kuondoa tatizo hilo.

''Jimbo la ubungo lilikuwa na viwanda vingi kama urafiki lakini sasa hivi vimedorora na vingine vimefungwa tunahitaji mtu atakayepiga kelele  kwa sababu vile viwanda bado maeneo yapo tunaweza kuleta wawekezaji vile viwanda vikafufuliwa'' amesema Kabendera

Aidha amesema njia hiyo itasaidia kupunguza changamoto ya ajira ambapo pia ameahidi kutoa mikopo ambayo itawasaidia kujikomboa kiuchumi