
Ushauri huo umetolewa na wadau wa sheria na uchambuzi wa siasa wakati wa mahojiano na EATV ambapo wamesisistiza uwepo wa sheria hiyo kuwa utasaidia kuendeleza sera chanya za ukuaji wa uchumi.
“Ukiangalia kila kiongozi utakuta ameweka mikakati ambayo ipo katika kuhakikisha kuna kuwa na uwezo wa kushindana na kuboresha uchumi kutoka katika utegemezi wa sekta moja pekee.” Henry Mwinuka Wakili
Kwa upande wake Wakili na Mchambuzi wa siasa Dkt. Onesmo Kyauke, amesema nchi zilizofanikiwa kufikia uchumi wa kati zimekuwa na mkakati wa uwekezaji katika sekta mseto ili kusaidia kuendelea kukuza sera zake na hivyo kupanda zaidi.
“Vipo vigezo vingine ambavyo vimewekwa katika dira ya maendeleo ikiwemo mikakati ya uboreshaji wa miundombinu,huduma mbalimbali ya kisekta.”
“Vyama vya siasa vituambie katika ilani zao namna ya utekelezaji,kukosa muongozo huo umeturudisha nyuma haswa katika elimu mfano sera ya UPE enzi za mwalimu Nyerere ambayo ilisaidia kwa zaidi ya asilimia 90,baada ya hapo hali ilibadilika kutokana tu na sera za serikali zilizoteuliwa” alisema Dkt Onesmo Kyauke