Picha ya Moyo
Ila tuangalie moyo kwenye upande wa burudani na mahusiano kama ambavyo wasanii wengi wa BongoFleva walivyolalamika kuhusiana na hilo kwenye nyimbo zao.
Moyo mashine - Ben Pol
Wimbo huu wa Ben Pol ulitoka mwaka 2016 ilifanya vizuri sana kwenye chati za muziki hapa Tanzania, mpaka sasa ina watazamaji Milioni 8 kwenye mtandao wa Youtube, kwenye ngoma hiyo Ben Pol ameusifu moyo wake hadi kuuita moyo mashine kwa kuvumilia, kuzungushwa, kusemwa na kutokata tamaa kutoka kwa mtu ambaye anampenda.
Usiusemee Moyo - Lady Jay Dee
Miaka 20 ya Komando Jide ina moyo wake pia ambapo mwaka 2003 alitoa wimbo wa usiusemee moyo wa mtu kama kujigamba kwa wengine kama anakupenda sana hali ya kuwa akitoka nje hujui alitendalo, wimbo huo ulishinda tuzo ya wimbo bora wa RnB kwenye tuzo za 'Tanzania Youth Achievements Awards'
Moyo wangu - Rose Muhando
Malkia huyu wa muziki wa Injili Tanzania aliimba wimbo kuhusiana na moyo ambapo amezungumzia kuwa moyo wake atamkabidhi Yesu na sifa zote atampa Yesu Kristo.
Moyo sukuma damu - Lameck Ditto
Alikuwa kimya kwenye game ila baada ya kuachia kazi ya moyo sukuma damu alirudi vizuri na alipokelewa vizuri kwa mashabiki wa muziki hasa wale waliotendwa kwenye mahusiano ambapo walitumia wimbo huu kama kufuta mawazo, kujiliwaza na kujipa moyo kuhusu mahusiano.
Moyo - Vanessa Mdee
Vanessa Mdee amelalamika sana kwenye huu wimbo wa moyo, tena aliachia kazi hii baaada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake msanii Juma Jux, Vanessa anasema moyo umemkosea sana kwani alimpa mtu ambaye hukumthamini, alimsaliti na mlevi, imepita mwaka mmoja sasa tangu Vanessa Mdee kutoka wimbo huo ambao ulipendwa zaidi na kina dada.
Mali yangu na Mbio - Alikiba
Kwenye nyimbo hizi mbili staa wa BongoFleva Alikiba aliiimba kuhusiana na moyo, kwanza kwenye wimbo wa mali yangu ambapo anasema kama alifanya makosa moyo wake kumpenda na kumchagua mwanamke ambaye alimsaliti.
Pia kwenye wimbo wa mbio akasema kupenda pasipo thamani kwa upande wake anaona sio sawa hivyo ni bora apewe moyo wake aufiche.