Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mambo matano kuhusu Shangazi Fatma Karume

Friday , 7th Aug , 2020

Kupitia kipindi cha SalamaNa inarushwa na East Africa TV kila Alhamisi kuanzia 3:00 usiku, Mwanasheria na Wakili wa kujitegemea Fatma Karume "Shangazi" amefunguka mambo mengi yanayomuhusu kuanzia siasa, sheria, familia, kazi na mahusiano.

Mwanasheria Fatma Karume "Shangazi"

Sasa haya hapa ni mambo matano ambayo ameweza kuyasema wakati anafanyiwa mahojiano na mtangazaji Salama Jabir "Ece Jay".

Kuvaa nguo nyeupe

Fatma Karume amesema ukiweka ahadi lazima utimize hivyo yeye ameweka nadhiri ya kuwa ataendelea kuvaa nguo nyeupe mpaka siku ya kupiga kura na hapendi kutofautishwa na wengine.

Vitu anavyopenda kuvifanya nje ya kazi zake 

Mimi Naweza kushona nguo zangu mwenyewe kwa kutumia Cherehani na najifunzia kwenye YouTube, napika udi mzuri, jam, nasoma sana hasa muda wa sasa na kazi yangu ya sheria inanifanya kusoma sana” amesema Fatma Karume 

Kadi ya uanachama 

Fatma Karume amesema hana kadi ya chama chochote pia hajawahi kuomba wala kusaini kutaka kuwa na chama chochote, pia ameongeza kusema ni uhuru wake kutaka kuwa na chama au la.

Kifo cha Babu yake Mzee Abeid Amani Karume

Kwenye familia yao wamezaliwa watoto 6 na yeye ndiyo mtoto wa kwanza kuzaliwa, kuhusu kifo cha Babu yake Mzee Abeid Amani Karume amesema alikuwa na miaka mitatu, na anaikumbuka hiyo siku lakini hakuwa na fikra za kuelewa wakubwa wanachofikiria.

Ofisi yake kupigwa Bomu 

Moja kati ya tukio baya lililomtokea ni ofisi yake kupigwa bomu mida ya saa 8 usiku mwezi August 2017 na mpaka leo hajapewa ripoti ya polisi nani aliyefanya tukio hilo.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine