
Rais Magufuli Bungeni
Katika hotuba yake, Rais Magufuli amesema, "Wakati tukiingia madarakani kulikuwa na wimbi kubwa la uhalifu wa kutumia silaha, pamoja na matukio ya mauaji kule Kibiti na kupitia Vyombo vya Ulinzi na Usalama vitendo hivyo vilikomeshwa na nipende kusema kuwa nchi yetu kwa sasa ni salama" - Rais
Aidha Rais Magufuli ameelezea namna ambavyo serikali yake imefanikiwa kuimarisha Muungano katika kipindi cha miaka mitano.
"Muungano wetu umeweza kuimarika tumewekeza kushughulikia baadhi ya changamoto za Muungano na kufikia mafanikio na makubaliano ikiwemo kuhusu suala la gharama za kushusha mizigo na pia kufuta kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na deni la shirika la umeme la Zanzibar lililokuwa likidaiwa na TANESCO, na hii yote ni katika kulinda Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar", amesema.
Pia amewashukuru marais wastaafu ambao pia wapo Bungeni. "Katika hilo ndugu zangu nawashukuru hawa viongozi wetu wakuu ambao ni mzee Mwinyi alijulikana kama Mzee Ruksa, Mzee Mkapa alijulikana kama Mzee Kweli, na Mzee Kikwete alijulikana kama Mzee wa Ari mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya".
"Tumeongeza idadi ya Shule za Msingi kutoka 16,899, hadi 17,804, Sekondari nazo zimeongezeka kutoka 4,708 hadi 5,330 vile vile tumekarabati shule kongwe 73 za Sekondari kati ya shule 89 na kujenga mabweni 253 na nyumba za maabara 227" - Rais @MagufuliJP#JPMKuvunjaBunge pic.twitter.com/zAmknXY29v
— EastAfricaRadio (@earadiofm) June 16, 2020
"Tumeongeza idadi ya Vituo vya kutolewa huduma za Afya 1,769, tumejenga Hospitali za Rufaa za kanda 3, tumeajiri watumishi wa Afya wapya 14,479, Madaktari 1,000, hii imeongeza idadi ya watumishi wa afya kutoka 86,152 hadi 100,631" - Rais @MagufuliJP#JPMKuvunjaBunge pic.twitter.com/IrJuaiveSd
— EastAfricaRadio (@earadiofm) June 16, 2020
Tazama #LIVE hotuba yake hapo chini