
Mbunge wa Lushoto Shabani Shekilindi
Shekilindi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Mwandishi wa EATV / EA Radio Digital, Sangu Joseph, ambapo amesema kupitia dawa hiyo ya tiba asili ameshawatibia wagonjwa zaidi ya 30 na wote wamepona.
"Mpaka dakika hii nimeponya wagonjwa zaidi ya 30 ambao wamepona Corona kupitia dawa yangu, na nilichokifanya nimezungumza na Waziri Mkuu ambaye alinikabidhisha kwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, ili kuipeleka Maabara kwa ajili ya uthibitisho wa kitaalam." amesema Shekilingi.
"Endapo Serikali itakubali juu ya dawa yangu, kwa sasa siwezi kusema itakuwa gharama shilingi ngapi, hilo nitawaachia Serikali, ila lazima gharama iwepo ili kusaidia utengenezaji" ameongeza Mbunge wa Lushoto Shabani Shekilindi.
Mbunge adai kugundua dawa ya Corona#VIDEO Mbunge wa Jimbo la Lushoto Shabani Shekilindi akizungumza na Mwandishi wetu @sangujoseph1 kuhusiana na namna alivyogundua dawa anayodai inatibu ugonjwa wa Corona.
Tazama zaidi : -https://t.co/GiHX5BFDjH pic.twitter.com/4FJlKeGdCH
— eastafricatv (@eastafricatv) May 8, 2020
Tazama video kamili hapo chini :-