Tuesday , 21st Apr , 2020

Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania (S.D.A), limetangaza marufuku kwa viongozi wake wakiwamo maaskofu na wachungaji, kutokusafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine ndani ya nchi, ili kuepuka maambukizi ya COVID 19.

Virusi vya Corona

Marufuku hiyo imetangazwa na Mkurugenzi anayehusika na mambo ya miradi ya Kanisa hilo nchini, Sessan Msafiri, katika ibada ya kuliombea Taifa kuondokana na ugonjwa hatari wa Corona, iliyofanyika Kanisa la Wasabato Sabasaba Tarime, Jimbo la Mara.

"Kama Kanisa kuna mambo mengi tumeyafanya ikiwemo kuzuia safari za viongozi kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine, nisisitize kuwa Tarime ikpo mkoani kwahiyo tunaweza kupokea wageni wengi kutoka Kenya", amesema Sessan Msafiri.

Pia Mkurugenzi huyo ametoa rai kwa kila muumini kuweka karantini nguo anazovua baada ya kufika nyumbani akitoka kazini.