Tuesday , 1st Oct , 2019

Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya TP Mazembe ambaye kwasasa anakipiga na klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji huku pia akiwa nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ametoa salamu za pole kwa timu ya TP Mazembe kufuatia kifo cha Makamu wa Rais.

Katika salam hizo Samatta ameeleza namna kuguswa na msiba huo huku akiweka wazi kuwa yeye pamoja na mashabiki na timu nzima ya TP Mazembe watamkumbuka daima Kwamwanya.

'Salam zangu za rambirambi ziwafikie familia, ndugu, jamaa, marafiki na timu nzima pamoja na mashabiki wote wa klabu yangu ya zamani ya TP Mazembe kwa kumpoteza Makamu wa Rais wa klabu ndugu Mohamed Kamwanya Ilunga', ameandika Samatta. 

Aisha Samatta ameongeza, 'Pumzika kwa amani Rais Kamwanya, tutakukumbuka daima'.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo, Kamwanya amefariki usiku wa kuamkia leo Oktoba 1, 2019 baada ya kuugua ghafla.

Samatta aliichezea TP Mazembe kuanzia mwaka 2011 hadi 2015, na kufanikiwa kutwaa mataji mbalimbali ikiwemo klabu bingwa Afrika, pamoja na kuwa mfungaji bora wa Ligi ya mabingwa mwaka 2015, mafanikio yaliyopelekea kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa ndani mwaka huo.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

LE TP MAZEMBE EN DEUIL Décès du 2ème vice-président KAMWANYA Le Tout Puissant Mazembe Englebert a le regret d’informer la famille sportive de la République Démocratique du Congo, du décès inopiné de son 2ème vice-président Mohamed KAMWANYA ILUNGA, mort survenue ce lundi 30 septembre vers 18h40. Mohamed KAMWANYA nous a quittés ce lundi 30 septembre des suites d'une très courte maladie. Il était depuis plusieurs années un membre fidèle et écouté de la direction du club et a été, à de très nombreuses reprises, le chef de délégation lorsque l’équipe se déplaçait sur le continent. Dimanche, il avait savouré, à la Kenya, la qualification d’un club qu’il chérissait profondément. Par respect pour la religion musulmane de l’illustre disparu, le TP Mazembe informe les amoureux du football que les funérailles auront lieu ce mardi 1er octobre 2019 selon le programme ci-après : - 11h30 : Recueillement à la morgue musulmane du Golf, sise Avenue de la Mosquée au quartier Golf Météo 1, référence arrêt Office des routes. - Il sera suivi de l’enterrement dans sa ferme privée sur la route de Kasumbalesa. Pour le Tout Puissant Mazembe Moïse KATUMBI CHAPWE, Président

A post shared by T.P Mazembe Englebert (@tout_puissant_mazembe) on