Mashabiki wa Taifa Stars baada ya mchezo wa jana huko Burundi.
Timu hiyo ya taifa ilipata sare ya 1-1 jana jioni kwenye mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2022 nchini Qatar.
— TFF TANZANIA (@Tanfootball) September 5, 2019
Sare hiyo ilipatikana kwa goli la kusawazisha dakika ya 85, lililofungwa na Simon Msuva baada ya Tanzania kuwa nyuma kwa goli 1-0 kutoka dakika ya 81.
Baada ya mchezo huo kikosi cha Taifa Stars kinatarajiwa kuwasili Dar Es Salaam leo saa 11:35 jioni, kwa ndege ya Air Tanzania.
Mchezo wa marudiano utapigwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es salaam Septemba 8, 2019.

