Saturday , 3rd Aug , 2019

Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili (DW) Mohammed Dahman, amefariki dunia siku ya jana ya Agosti 2, 2019 Jijini Cologne, magharibi mwa Ujerumani.

Aliyekuwa mtangazaji wa DW, Mohamed Dahman

Taarifa hizo zimetolewa na Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya DW, Andrea Schmidt, akisema kuwa Dahman alikuwa ni mwandishi bora na alipendelea sana kusoma taarifa ya habari za ulimwengu na makala ya mbiu ya mnyonge.

Aidha taarifa hiyo imebainisha kuwa,  Dahman alikuwa akiugua kwa kipindi cha takribani miaka miwili na muda wote huo hakuweza kufanyakazi. DW imepeleka pole za dhati  kwa mke wake, binti yake na familia yake visiwani Zanzibar na ughaibuni.