Friday , 16th May , 2014

Taasisi ya utafiti wa masuala ya afya na tiba ya Ifakara Health Institute imesema kuna uwezekano virusi vya homa hatari ya Dengue vimeingia nchini kutoka nchi za Asia na Amerika ya Kusini ambako ugonjwa huo upo kwa siku nyingi.

Aidha, taasisi hiyo imesema kuwa tofauti na ambavyo imekuwa ikielezwa kuwa mbu anayesambaza homa ya Dengue huwa anang'ata nyakati za usiku, taasisi hiyo inafahamu juu ya uwepo wa mbu aina ya Aedes Afrikanus ambaye hung'ata wakati wa usiku na ambaye pia husambaza homa ya Dengue.

Mtafiti mwandamizi ambaye pia ni mkuu wa idara ya Malaria na tabia za mbu wa kituo hicho Dkt. Nicodemus Govella, amesema hayo katika mahojiano na East Africa Radio ambapo amesema kwa sasa taasisi hiyo inakusanya pesa kwa ajili ya kufanya utafiti utakaobaini idadi ya mbu wenye ugonjwa huo, maeneo waliyopo, tabia zao na jinsi ambavyo nchi inaweza kukabiliana na ugonjwa huo.