Monday , 5th Dec , 2016

Mbunge mmoja nchini Uingereza amesema kuwa mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anafaa kuchunguzwa na maafisa wa Uingereza kufuatia madai kwamba alitumia kampuni za kigeni kupunguza kodi anayolipa.

Jose Mourinho

 

Mourinho anashutumiwa kwa kuhamisha mamilioni ya pauni za Uingereza hadi kisiwa kinachomilikiwa na Uingereza cha Virgin Island ili kukwepa kulipa kodi.

Hata hivyo wakala wake amesema kuwa madai hayo hayana msingi wowote.

Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za mali ya umma Meg Hillier aliambia Gazeti la Sunday Times kwamba madai hayo yanafaa kuchunguzwa.