
Mkuu wa majeshi nchini Tanzania, Davis Mwamunyange.
Akizungumza mara baada ya kufungua mkutano wa nane wa wakaguzi wakuu wa majeshi ya nchi za SADC unaoendelea jijini Arusha Jenerali Mwamunyange amesema ukaguzi huo unasaidia majeshi hayo kuwa tayari wakati wote.
Mkuu huyo wa majeshi amesema kupitia mikutano ya umoja wa wakaguzi hao wa majeshi ya SADC tayari kumekua na makubaliano ya kuwa na taratibu zinazoshabihiana katika ukaguzi.