Friday , 17th Jun , 2016

Mkazi wa kijiji cha Wavu kata ya Shabaka wilayani Nyang'hwale mkoani Geita Shilinde Mbushi [41] akishirikiana na mwanaye Ndebile Shilinde [21] anadaiwa kumuua dada yake Kweji Mbushi [40]

Mponjoli Rodson Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita

Mkazi huyo anatuhumiwa kufanya mauaji hayo kwa kumkata kata kwa kitu chenye ncha kali na kutenganisha kichwa na kiwiliwili chake na kisha kutoweka na kichwa chake June 8 saa nne za usiku kabla ya kichwa hicho kupatikana juzi na watuhumiwa tayari wanashikiliwa na polisi.

Kamanda Mponjoli Rodson amefafanua kuwa kichwa cha marehemu Kweji kilipatikana juzi kikiwa kimetelekezwa huku akitoa rai kwa jamii kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mikononi.

Mponjoli Rodson Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita anazungumzia tukio hilo la kikatili wa aina yake, Msikilize hapa:-