
Harusi ya msanii huyu itafanyika siku ya Jumamosi, tarehe 26 baada ya ile ya kimila ambayo ilifanikiwa vilivyo kuviteka vichwa vya habari mwezi Novemba mwaka jana.
Wawili hawa wanatarajia kuweka historia nyingine kubwa kwa kufanya sherehe ya kifahari, wakifuata nyayo za 2face Idibia na mkewe Anie Macaulay ambao walifunga ndoa nchini humo mwezi Mei mwaka jana.