Baadhi ya viongozi wa UKAWA, James Mbatia kutoka NCCR Mageuzi na Freeman Mbowe wa chama cha demokrasia na maendeleo - Chadema
Wakiongea na Watanzania kupitia vyombo vya habari jijini Dar es salaam leo wanafunzi hao walioongozwa na kiongozi wao Dorcas Mwasunda wamesema kuwa wao kama wasomi wameona ni vyema kukosoa kile kinachoendelea nchini kwa kutumia kile walichokiita Uhuru wa kitaaluma.
Wanazuoni hao pia wamelaani vitendo vingine vinavyoendelea katika bunge maalum la katiba ikiwa ni pamoja na kudhalilishwa kwa waasisi wa Taifa Wanazuoni pamoja na wanataaluma nchini, huku wakishindwa kutambua kundi la wanasiasa lililounda umoja unaoitwa UKAWA bungeni.

