Kocha msaidizi wa Timu hiyo Edna Lema amesema, japo safari ilikuwa ikiahirishwa kila mara lakini kwa upande wao haijaathiri chochote kwani walikuwa wakiendelea na maandalizi ya michuano hiyo na wanaamini ushindi utapatikana kwa jitihada walizonazo.
Kocha Edna amesema, mchezo wao wa kwanza dhidi ya Ivory Coast hapo Septemba sita wanaamini watafanya vizuri kwani kinachotakiwa ni ushirikiano baina ya wachezaji ili kuweza kufanya vizuri.
