Wednesday , 2nd Sep , 2015

Star wa muziki wa Genge, Frasha wa nchini Kenya amekuwa ni moja kati ya watu mashuhuri walioonesha wazi kumsapoti Gavana wa Machakos nchini humo, kufuatia kitendo chake cha kumwaga chozi hadharani mwishoni mwa wiki kwa madai ya kufitiniwa na wakubwa.

Frasha

Frasha ameeleza kuwa, yeyote anayempinga gavana huyo Dk. Alfred Mutua na mkakati wake unaotambulika kama maendeleo 'Chapchap', ni adui wa maendeleo, akisisitiza kuwa katika wakati huu wa changamoto kwake yupo pamoja naye.

Mbali na hilo kwa sasa Frasha ambaye pia amejikita kuendesha project pembeni ya kundi, anafanya vizuri katika chati kupitia kolabo aliyofanya na Timmy Tdat na Mchizi Gaza, kazi ambayo unaitazama sasa kupitia eNewz ikiwa inasimama kwa jina “Shigidi”.