
Gladys Cherono na Eliud Kipchoge
Katika mbio hizo kubwa na zenye heshima duniani zilizofanyika leo Kipchoge, ametumia saa 2:01:39 kukimbia kilomita 42.195 hivyo kuvunja rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Mkenya mwingine Dennis Kimetto ambaye alitumia saa 2:02:57 mwaka 2014.
Kwa upande wa wanawake mwanariadha Gladys Cherono wa Kenya ameshinda baada ya kutumia saa 2:18:11. Cherono sasa anakuwa mwanariadha wa 4 duniani kwa upande wanawake kutumia muda mfupi zaidi kumaliza mbio hizo.
Kipchoge anatajwa kama mwanariadha bora zaidi kuwahi kutokea kutoka na mafanikio yake ambapo mapema mwaka huu alishinda mbio za London Marathon kwa mara ya tatu huku pia akiwa ni bingwa wa olimpiki wa mbio ndefu.
Katika mbio za leo kwa wanaume, Kenya imefanikiwa kuchukua nafasi zote tatu za juu ambapo wanariadha Amos Kipruto na Wilson Kipsang wameshika nafasi za pili na tatu.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, amewapongeza wanariadha hao kwa ushindi wao.
Congratulations @EliudKipchoge for breaking the world record at the #BerlinMarathon2018. I also congratulate his compatriots Amos Kipruto & Wilson Kipsang' for going out valiantly to bring a 1-2-3 victory for #TeamKenya. You are our heroes. Kenya is proud of you. pic.twitter.com/qOuQoC5dZZ
— Uhuru Kenyatta (@UKenyatta) September 16, 2018