mashindano ya wazi ya Australia
Katika mchezo huo wa mzunguko wa kwanza Murray atakuwa akiwania kushinda ili asonge mbele zaidi akiwania ubingwa wa michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kupoteza katika fainali nne zilizopita ikiwemo ya mwaka jana dhidi ya Novan Djokovic.
Kwa upande wake bingwa mtetezi ambaye pia ndiye kinara kwa ubora duniani Mserbia Novan Djokovic ataumana na mchezaji waia wa korea kusini Hyeon Chung katika mechi yake ya kwanza.
Kwa upande wa wanadada bingwa mtetezi wa michuano hiyo Serena Williams amepangwa kwenye kundi gumu ambapo ataanza kampeni za kutetea taji lake dhidi ya muitalia Camila Giorgi.

