Rais wa TPBO Yasin Abdalah ustaadh akiongea kwaniaba ya wasimamizi wa pambano hilo PST amesema kimsingi maandalizi yote yamekamilika kwa kiasi kikubwa huku baadhi ya mabondia wa utangulizi toka mkoani Tanga nao wakiwasili jijini Dae es salaam hapo kesho
Huku pia Ustadh akiwataka mabondia wote kufika kwa wakati hasa siku ya ijumaa siku ambayo kutafanyika zoezi la mwisho kabisa la upimaji uzito kwa mabondia wote watakaovaana siku ya jumamosi march 29 katika ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam.