Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kocha wa zamani wa Yanga aomba kazi Singida United

Saturday , 26th May , 2018

Baada ya hivi karibuni kuongea na East Africa Television na kuthibitisha kuwa wanaachana na kocha wao Hans Van Pluijm, Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga, leo ameweka wazi kuwa wamepokea maombi ya kocha wa zamani wa Yanga Dusen Kondic.

Sanga amesema bado wanapitia wasifu wa makocha mbalimbali kutoka maeneo tofauti ambao wameomba kuchukua mikoba ya Hans ambaye anaondoka klabuni hapo baada ya mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Mtibwa Sugar Juni 2.

''Mpaka sasa hatuna uhakika wa nani atachukua nafasi ya Hans, lakini tutatangaza hivi karibuni baada ya watalaam wetu wa masuala ya ufundi kumaliza kazi ya kupitia majina yaliyoomba kazi, akiwemo kocha wa zamani wa Yanga Mserbia Dusen Kondic pamoja na wengine wa nje na hapa kwetu'', amesema.

Dusen Kondic alijiunga na Yanga November 2007, akichukua mikoba ya Mserbia mwenzake Sredejovic 'Micho' Milutin.  Hata hivyo hakudumu ndani ya klabu hiyo kwani alifutwa kazi mwishoni mwa msimu wa 2007/08.

Singida United ambayo imerejea ligi kuu msimu huu, imeonesha ushindani mkubwa ambapo hadi sasa ipo katika nafasi ya 5, ikiwa imesalia mechi moja kumalizika kwa msimu. Timu hiyo pia inaweza kupata nafasi ya kuwakilisha nchi endapo itaifunga Mtibwa Sugar kwenye fainali ya FA Juni 2.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine