Akizungumza na East Africa Radio, Afisa habari wa BMT, Najaha Bakari amesema, baada ya kuchagua viongozi wa muda watapanga tena tarehe ya uchaguzi wa chama hicho ambapo walewale waliochukua fomu ndio watakaoshiriki uchaguzi huo.
Uchaguzi wa Badminton ulitakiwa kufanyika Juni 10 mwaka huu lakini uliahirishwa tena baada ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kushindwa kufika katika uchaguzi huo.
