Tuesday , 22nd Jan , 2019

Baada ya Yanga kutolewa kwenye michuano ya SportPesa na Kariobangi Sharks kwa kufungwa mabao 2-3, msemaji wa Simba Haji Manara amesema yote amesababisha Jacob Massawe ambaye alivunja mwiko wa Yanga kutofungwa msimu huu.

Mashabiki wa Yanga

Yanga imetolewa katika mchezo wa kwanza ambapo michuano hiyo huanzia hatua ya robo fainali. ''Kwasasa imekuwa rahisi tu Yanga kufungwa baada ya Jacob Massawe kuwafunga'', amesema Manara.

Yanga sasa imeungana na Singida United kuwa timu mbili ambazo zimeaga mashindano ya SportPesa baada ya Singida United kufungwa bao 1-0 na Bandari FC kwenye mchezo wa mapema leo.

Mabao ya Kariobangi Sharks yamefungwa na Abuya Duke aliyefunga mawili pamoja na Abege George aliyefunga moja. Huku yale ya Yanga yakifungwa na Amissi Tambwe na Heritier Makambo.

Kesho Simba itashuka dimbani kucheza na AFC Leopard huku mabingwa watetezi Gor Mahia wakicheza na Mbao FC ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza.