Monday , 26th Jan , 2015

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara amesema kuwa amefurahishwa na jitihada za kampuni ya Tigo katika kuanzisha mfumo unaotoa nafasi nyingine mpya kwa wasanii wa muziki kufaidika na kazi wanazofanya.

Tamasha la muziki la Tigo Kiboko Yao Leaders Club jijini
Dar es Salaam

Mhe. Dkt. Fenella amesema haya wakati akizindua rasmi huduma ya Tigo Music jumamosi hii katika tamasha la Kiboko Yao, ambapo amesema kuwa Wizara yake ipo tayari kushirikiana na sekta hizi binafsi zinazoonyesha jitahada katika kuendeleza sanaa.

Huduma Ya Tigo Music itawawezesha wateja wa huduma za mtandao huo kupata nyimbo milioni 36 za wasanii wakitanzania na Afrika kwa ujumla katika simu zao za mkononi za Smartphone.