
Mratibu wa mashindano hayo kutoka BASATA, Kwerugira Maregesi
Maregesi ametaka madansa wanaounda makundi hayo kuongeza mazoezi na juhudi kutokana na ukubwa wa mashindano hayo Afrika Mashariki, kufahamu kuwa hii ndio nafasi ya wao kuonekana na kupata mashavu ya kibiashara, ubunifu na mitindo mipya ikiwa ndiyo siri pekee ya kufanikiwa kusonga mbele.
Maregesi pia ameeleza kufurahishwa na kuzidi kupiga hatua kwa mashindano hayo akiwataka madansa pia kulizoea jukwaa jipya na bora ambalo limeanza kutumika kama sehemu ya maboresho ya mashindano.
