Tuesday , 31st Jan , 2017

Msanii wa nyimbo za Injili Christina Shusho amesema wasanii wa nyimbo za Injili hawana tabia za kuongea uongo wala maisha ya kuigiza katika maisha yao ya umaarufu.

Christina Shusho

 

Akiongea kupitia eNewz ya EATV, Shusho amesema wasanii wa nyimbo za injili wanapenda kuishi maisha yao halisi siku zote na hawapendi kuingiza maisha ambayo siyo yao ili kuwadanganya mashabiki zao wanaowafuatilia kwamba wanaishi maisha mazuri wakati siyo kweli.

Pia Shusho amesema watu maarufu wanapaswa kutambua kwamba kuna watu ambao wanafuatilia kila kitu wanachokifanya  katika maisha yao hivyo wanawaharibia maisha wanapowadanganya  mashabiki wanaowafatilia