Tuesday , 1st Apr , 2014

Baada ya kuwekeza nguvu nyingi katika kutengeneza video ya ngoma yake kali inayofahamika kwa jina, 'Wanatetemeka' msanii Queen Darlen, hatimaye msanii huyu amepanga kuiachia rasmi kazi hii Jumapili tarehe 6 mwezi huu Jijini Dar es Salaam.

Wanatetemeka Video Set

Kazi hii ikiwa kama moja ya projekti kubwa kabisa kwa Queen Darleen kuwahi kufanya, ndani yake akiwa ameshine vilivyo na Msanii Diamond Platinumz ambaye ni kaka yake wa damu, eNewz imepata nafasi ya kumegewa kipande kifupi tu cha kazi hii kutoka kwa muongoza video yenyewe Jerry Mushala ambacho utapata kukitazama katika show leo saa mbili kasoro usiki EATV pekee.