Wednesday , 27th May , 2015

Staa wa filamu Hashim Kambi, ambaye anafanya vizuri katika tasnia hiyo kwa miaka 10 sasa, amekiri kuwepo na uchache wa waigizaji wa makamu yake katika tasnia hiyo, hali iliyotengenezwa na imani potofu kuwa uigizaji ni uhuni katika kipindi cha nyuma.

Hashim Kambi

Hashim amesema kuwa, binafsi alishawishiwa kuanza kuigiza baada ya nafasi za uhusika wa watu wazima katika filamu kuwa zinafanywa na watoto, hivi sasa kukiwa na watu wazima wasiozidi watano katika tasnia hiyo nzima.

Hashim Kambi amesema kuwa kwa sasa hali imekuwa tofauti baada ya watu kuanza kuona umuhimu na nafasi ya sanaa katika jamii, ambapo watu wa rika tofauti wameendelea kufunguka na kushiriki katika tasnia hiyo.