
Rama Dee amebainisha hayo katika kipindi cha KIKAANGONI ambacho kinarushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mpaka saa kumi jioni.
“Lowasa anapaswa apumzike awaachie watu wafanyekazi…Kwa kawaida umri wa wazee wetu wakifika umri wa miaka 55 au 60 ni umri wa kupumzika kwa kuwa wamekuwa tayari wamezeeka”. Alisema Rama dee
Aidha, Rama dee aliendelea kusema kuwa Mhe. Lowassa kwa sasa anapaswa atafute mtu wa kumrithi nafasi yake nasiyo kuendelea tena katika harakati za masuala ya kisiasa na mengineyo.
“Nafikiri yeye angeweza ku-focused kwa kumtafuta mtu ambaye ataweza kuishika ile nafasi yake naimani itakuwa vizuri zaidi”. Aliendelea kusema Rama dee