
Wakazi amefunguka hayo kutokana na watu kuhoji kutokuwepo kwa wasanii hao ambao ni watu wakaribu zaidi kwao na kufafanua kwamba hawakuwahi kumfikiria Nikki Mbishi kuwa sehemu ya kundi lao kwa sasa kwani kibiashara haitaweza kuwanufaisha.
"Kibiashara hatukuwahi kumfikiria Nikki Mbishi lakini One Incredible alikuwepo kwenye orjino ya 'SSK' lakini pia waliungana na kina Stereo kutengeneza kundi lao linaloitwa 'Sisi' kwa hiyo kibiashara haipo sawa huwezi kuwa na makundi mawili yote yanaanza na sisi, tutaangalia kwanza kama haitoathiri biashara basi watakuja kujiunga hapo baadae inategemea na sapoti ambayo tutakuwa tunaipata." -Wakazi
SSK ni kundi ambalo linaundwa na Wakazi, P The Mc , Cjamoker pamoja na Zaiid ambao wameamua kufanya kazi kwa pamoja ili kuweza kurudisha asilimia 50 ya mapato wanayopata kupitia muziki wao katika jamii inayowazunguka.
Mtazame hapa chini Wakazi akitoa sababu.