
Msanii wa Bongo Fleva Vanessa Mdee
Wasanii hao ambao walikuwa wakionekana wakijibizana katika mitandao ya kijamii pasipo na kufahamika chanzo cha ugomvi wao juzi waliamua kulishana ugali jukwaani kwa mahaba yote ili kuwadhihirishia mashabiki wao kuwa zote zile zilikuwa ni promo tu za shoo yao.
Pia Msanii Kr Mulla aliamua kufunguka wazi kuwa kama asingelikuwa msanii yeye sasa angekuwa ni mtu wa kuiba mifukoni mwa watu tofauti tofauti ambao wangelikuwa wanamkalia sawa katika taimingi zake.