
Kundi la J Combat Crew kutoka Zanzibar lilipokuwa likionyesha vipaji katika uwanja wa Don Bosco Upanga Dar es salaam
Kwa mujibu wa mratibu wa shindano hilo Bhoke Egina usaili wa Chang’ombe utakuwa ni wa mwisho ili kupisha hatua ya robo fainali, nusu fainali na fainali yenyewe kwa watakaofanikiwa kusonga mbele.
‘’Usaili wa tarehe 30 utakuwa ni usaili wa mwisho ambapo makundi matano yatachaguliwa katika usaili huo na baada ya hapo yataungana na makundi mengine yaliyoshinda usaili wa kwanza na wa pili ili kutafuta watakaofuzu hatua ya robo fainali’’ Amesema Bhoke Egina
Dance100% inarushwa na kituo cha EATV kila siku ya Jumapili saa moja jioni chini ya udhamini wa Vodacom na Coca-Cola.