Roma Mkatoliki
Roma Mkatoliki kwa kuanza alimtaja Rapa Roho Saba na kusema anamsikiliza sana na kumkubali sana na watu watashangaa kwanini amemtaja Roho Saba ili hali ana ngoma mbili tu ila yeye anasema anazisikiliza sana hizo kazi mbili kuliko kazi nyingine nyingi kutoka kwa wasanii wengine.
"Kiukweli nawasikiliza sana wasanii wengi wa Hip hop Bongo lakini kwa kuwa nimepewa nafasi ya kutaja wasanii watano tu wa kwanza nitaanza na mwanangu Jaco Roho Saba, mchizi ana ngoma mbili tu lakini nazisikiliza sana, namkubali sana Jose Mtambo, Prof Jay pia maana kitambo namsikiliza na alini'inspire' toka enzi hizo mpaka leo. Wengine ni Saigoni pamoja na Hashim Dogo" alisema Roma Mkatoliki