Wednesday , 22nd Jun , 2016

Msanii wa bongo fleva Nisha anategemea kuwafuturisha watu wasiojiweza tarehe 26/6/2016 viwanja vya Azania Lego ili kuweza kuwasaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu na wasiojiweza ikiwa kama moja kati ya sadaka zake ambazo atakuwa ametoa

NISHA

Pia ameendelea kusema kwamba futari hiyo haina masharti, hivyo anawaalika watu wote bila kujali dini kuweza kujumuika na yeye katika siku hiyo ya kufuturisha kwani sadaka yake hiyo haana idadi wala kiwango cha watu ambao wanatakiwa kuwakilisha siku hiyo.

Hata hivyo Nisha ameendelea kusema kuwa wanategemea kuwa na viongozi mbalimbali katika kukamilisha futari hiyo akiwe Mama Samia Hassan na wengine, na kusema kuwa watu mbalimbali wajitokeze kusaidia watu wasio jiweza na si kwa mwezi mtukufu pekee bali katika nyakati zote