Monday , 14th Dec , 2015

Msanii wa muziki Mrisho Mpoto, moja ya nyota wanaoiwakilisha Tazania kuwania tuzo kubwa Afrika za Kora, amekuwa ni sehemu ya wahamasishaji katika jitihada za kupambana na tatizo la lishe duni kwa asilimia kubwa ya watanzania hususan kundi la watoto.

Msanii wa muziki Mrisho Mpoto

Mpoto ameeleza kuwa, shughuli hiyo imemfikisha sehemu mbalimbali hususan vijijini kuelimisha makundi ya watu, hususan wakina mama kuchukua muda zaidi kufikia miaka 2 kunyonyesha watoto wao, ili kuwafanya wawe na afya na lishe bora kama anavyoeleza hapa.