Saturday , 28th Jun , 2014

Mchekeshaji maarufu Mboto Haji ameweka peupe swala zima la mahusiano yake ya kimapenzi kwa sasa, ambapo amewataka mashabiki wake kufahamu kuwa, yeye ana mtu ambaye hakupenda kutoa taarifa zake za ndani na pia amejaliwa kupata mtoto mmoja.

Mboto Haji

Mboto amesema kuwa, anapendana sana na mpenzi wake huyu isipokuwa katika swala la kuoa, bado ni mapema kufanya hivyo kutokana na imani yake kuwa mambo haya hayahitaji haraka.

Pembeni ya ishu ya maisha binafsi ya Mboto, Msanii huyu pia amegusia kuwa na kazi mpya na kubwa ya filamu ambayo ameifanya na Marehemu Rachel Haule aliyefariki hivi karibuni, ambayo anatarajia kuiachia hivi karibuni kati ya kazi nyingine kali.

Tags: